Simba wanaongoza goli 2 Es Satif hawajapata kitu mpaka sasa mpira unaendelea

Mshambuliaji wa Timu ya
Simba,Salum Machaku (kulia) akijiandaa kuachia shuti kali kuelekea langoni mwa
timu ya Es Satif katika mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho unaoendelea
hivi sasa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Timu ya Simba SC
inaongoza goli 2 wakati Es Satif hawajapata kitu mpaka sasa,Goli la
kwanza limefungwa na mchezaji Emmanuel Okwi na goli la pili limefungwa na Haruna
Moshi a.k.a Boban.
Mshambuliaji wa
Simba,Emmanuel Okwi (kulia) akimtoka beki wa timu ya Es Satif ya nchini
Argeria,Farouk Belkaid katika mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho
unaoendelea hivi sasa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha Simba.
Kikosi cha Es Satif
Marefarii na Manahodha wa timu zote mbili.
Mkono wa kheri kabla ya mtanange kuanza.
Ameir Maftah wa timu ya Simba (kulia)
akiachia shuti kali kuelekea langoni mwa timu ya Es Satif.
Beki wa Es Satif (alielala chini)
akiondosha hatari langoni mwake wakati Salum Machaku akitaka kujaribu kufunga
goli.
Holaaaaaa..........
Hatari langoni mwa Es Satif.

Waziri Mkuu mstaafu,Mh. Fredrick Sumaye (mwenye
suti),Waziri wa Afrika Mashariki,Mh. Samuel Sitta (kulia),Mbunge wa Jimbo la
Kigoma Kaskazini,Zitto Kabwe pamoja na Mbunge wa Tabora Mjini,Mh. Aden Rage
wapo uwanjani hapa kuisapoti timu ya Simba.
Mashabiki wa Simba wakiwa wamefurika
uwanjani hapa.
leo hapatoshi uwanja wa taifa kati ya simba sc na Es Setif ya Algeria
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0

Pichani ni kundi la Wanachama wa Simba kutoka Makao Makuu
wanajiita "SIMBA SPORTS CLUB MAKAO MAKUU TAWI LA MAENDELEO" Hapa ni
shamra shamra zinazoendelea nje ya uwanja wa taifa kabla ya kuingia uwanjani
hivi punde.

Leo ndio leo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam pale
Simba inapokutana na ES Setif kutoka Algeria katika mchezo wa Kombe la
Shirikisho. Simba inarekodi nzuri ya kuwafunga warabu hao kutoka Algeria. Hadi
sasa inarekodi ya 3-0.
Mmoja
wa Wakurugenzi wa Prime Time promotions Ltd ambao ndiyo waratibu wa mchezo huo
,Bw.Godfrey Kusaga akizungumza na Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage
kuhakikisha kuhakikisha kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa na Mashabiki
wanaingia uwanjani bila matatizo.
Wewe....nini picha zote hizo..!!!Hapa akimkoromea mpigapicha
kwanini anampiga picha nyingi....hahaha alipogundua ni Father Kidevu akabaki anacheka.
Mashabiki wakiwa tayari uwanjani kwa utulivu mkubwa wakisubiri
game kuanza na mnyama kumrarua mwarabu. Father Kidevu Blog ipo Live kukurushia
mtanange huu wa Simba na ES Setif kutoka Algeria.
jicho la camera ya jiachie nje ya jiji la dar
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Mteja akiulizia bei ya nyanya,ndoo moja inauzwa shilingi
8000/=
Urithi wetu wa kujivunia ndani ya hifadhi ya Wanyama Mikumi.
Mdau nae akikimbiza mpango mzima mapema sokoni ndani ya
Iringa.
Nchi yetu nzuri ya milima na mabonde ya kuvutia
Unajua ni kwanini
nazi inavunjiwa sokoni na si mara baada ya kufika nyumbani kwa matumizi.
Mchicha bila maji hauuziki;Mama akiwa na mtoto wake akiuza mboga
mboga soko kuu la mjini Iringa hivi karibuni.
semina elekezi ya msimy wa mashindano ya ya copa coca cola 2012 yafunguliwa jijini dar
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Mkurugenzi wa Michezo katika wizara ya Habari Utamaduni na
Michezo, Leonard Thadeo, akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina elekezi ya msimu
wa mashindano ya Copa Coca Cola 2012 kwa Makatibu wa vyama vya Mikoa jijini Dar
es Salaam jana. Kulia ni wa Rais wa Shirikisho la Soka (TFF) Athuman Nyamlani
na Meneja uhusiano na Makamu Mawasiliano wa Kampuni ya Coca-Cola Kwanza,Evance
Mlelwa.
Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka (TFF) Athuman
Nyamlani,akizungumza wakati ufunguzi wa semina elekezi ya msimu wa mashindano
ya Copa Coca Cola 2012 kwa Makatibu wa vyama vya Mikoa jijini Dar es Salaam
jana mashindano ya Copa Coca Cola 2012 kwa Makatibu wa vyama vya Mikoa jijini
Dar es Salaam jana.Katikati ni Mkurugenzi wa Michezo katika Wizara ya
Habari Utamaduni na Michezo Leonard Thadeo na Meneja uhusiano na
Mawasiliano wa Kampuni ya Coca-Cola kwanza,Evance Mlelwa.
Mkurugenzi wa Ufundi na Afisa Maendeleo wa Shirikisho la Soka(TFF)
Sunday Kayuni,akizungumza wakati ufunguzi wa semina elekezi ya msimu wa mashindano
ya Copa Coca Cola 2012 kwa Makatibu wa vyama vya Mikoa jijini Dar es Salaam
jana .
rais kikwete amteua Kibelloh kuwa Mwenyekiti KADCO
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Na mwandishi wetu
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amemteua
Balozi mstaafu wa Tanzania nchini Uingereza, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh
kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni inayosimamia maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa
Kilimanjaro (KADCO).
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Uchukuzi leo inasema kuwa uteuzi
huo ulianza kazi toka mwezi Machi tarehe 15. Aidha, taarifa hiyo pia
ilisema kuwa Waziri wa Uchukuzi, Mh. Omari Rashid Nundu kwa mamlaka aliyonayo
amewateua wajumbe wanne wa bodi ya wakurugenzi ya KADCO. Wajumbe hao wanne ni
pamoja na Seleman O. Seleman, Andrew Nyumayo, Mwajuma Mwanilwa na van de Kreeke
ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa KADCO.
Uteuzi huo wa bodi umekuja wakati KADCO ikiwa katika mipango ya
uboreshaji na ukarabati wa Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kuwa uwanja
wa ndege unaowezesha ndege kubwa za kimataifa kutua.
Kampuni ya KADCO imepata mkopo wa dola za kimarekani 35 milioni
(zaidi ya 47 bilioni) kutoka kampuni ya nchini Uholanzi, Orion Grand
Facility. Mkopo ambao utasaidia katika ukarabati mkubwa wa uwanja wa ndege
na maeneo mengine muhimu ya uwanja.
Hivi karibuni, Qatar Airways ilitangataza mpango wa kutua katika
uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa kutumia ndege kubwa ya A320
kupitia Nairobi, Kenya kuanzia mwezi Julai mwaka huu.
Mashirika mengine ya ndege
yanayotumia uwanja wa KIA ni pamoja na KLM, Edelweiss Air, Condor Air na
Shirika la Ndege la Ethiopia.
Katizo la umeme DSM, maeneo yatakayokatizwa Jimbo la Ubungo
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Jumapili tarehe 25 Machi
kutakuwa na katizo la umeme kwenye baadhi ya maeneo ya DSM kuanzia saa 2
Asubuhi mpaka 10 jioni.
Kwa Jimbo la Ubungo
katizo litahusu maeneo yafuatayo: Sinza, Goba, Ubungo Kisiwani, Mabibo Jeshini,
Makuburi (External, Barabara ya Mandela, Mabibo Hosteli, Kibangu).
Hivyo usishike waya
wowote uliokatika badala yake toa taarifa kwa ofisi za kanda za TANESCO Kinondoni
Kaskazini (Mikocheni):0716768584; 0784768584 au Kinondoni Kaskazini (Magomeni):
0768985100; 0784271461; 0784078837 au 0788379696.
Sababu zilizotajwa na
TANESCO: Kuunga line ya msongo mkubwa wa 132kV katika kituo cha kupoozea umeme
Ubungo na Kufunga LBS kwenye njia ya FZ3-1&2 na U1 ili kurahisisha uzimaji
wa line wakati inapopata hitilafu na kurahisisha kugundua eneo la hitilafu kwa
urahisi na haraka. Maslahi ya Umma Kwanza.
Mh Zitto Kabwe:Kwanza niseme wazi kabisa kabisa kuwa Urais ninautaka.
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Ninaamini ninao uwezo
wa kuwa Rais. Ninaamini nina uzalendo wa kutosha na utashi wa kuleta mabadiliko
stahili wa namna nchi yetu inavyoongozwa. Ninajua kuwa nchi yetu imesahau
maendeleo ya watu na kujikita katika maendeleo ya vitu. Ninajua kuwa hivi sasa
viongozi wetu wengi wanaangalia zaidi mitindo (styles) badala ya mambo ya
msingi (content). Ninajua kuwa maendeleo vijijini yamesahaulika.
Ninajua nchi yetu
inahitaji Uongozi wa kufanya mabadiliko makubwa (transformation) badala ya
mabadiliko ya juu juu (cosmetic change). Ninajua ‘transformation’ inahitaji
maamuzi magumu yatakayoudhi wengi na hasa mabwana wakubwa wa nchi za magharibi
mfano kuzuia nchi yetu kuuza malighafi tu. Ninajua rushwa, ufisadi na
ubadhirifu wa Mali ya Umma ni kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu na kwamba
lazima hatua madhubuti zichukuliwe kuzuia na kutokomeza ufisadi. Ninajua
rasilimali kama Madini, Mafuta na Gesi, Ardhi n.k. ni lazima zifaidishe
wananchi wa nchi yetu.
Hivyo, nchi inahitaji
Kiongozi wa juu atakayekabili changamoto hizi. Ninaamini ninaweza kuwaongoza
Watanzania wenzangu kukabili changamoto hizi. Sio kazi rahisi lakini ni kazi
ambayo lazima Mtanzania mmoja aifanye. Mimi nataka kuifanya. Nina uwezo wa
kuifanya.
Hata hivyo kazi hii
hata kama naitaka ni lazima wenye nchi waamue kunipa kazi hii. Ni lazima kwanza
Chama changu kiseme wewe ndio mwanachama unaestahili kuifanya kazi hii. Ni
lazima Watanzania wengi waseme wewe ndio mwananchi mwenzetu unayeweza kuchukua
jukumu hili. Kuitaka tu haitoshi. Ni lazima wananchi wakuamini na kukupa jukumu
hili.
Sasa kama wananchi
watasema huyu Zitto anapaswa kubeba jukumu hili mwaka 2015 tuache iwe. Kama
watasema hapana wewe bado mpaka mwaka 2020 au hata 2025 tuache iwe hivyo. Pia
Kama hawataki kabisa tuache iwe hivyo.
Mjadala wa umri wa
kugombea Urais imekuwa mjadala mkali sasa. Mjadala huu baadhi ya watu kwa
sababu wanazojua wao wameamua kuita ni mjadala wa Zitto na January. Kwamba ni
mjadala unaobagua Wazee. Mjadala unaopandikiza chuki na sumu za kibaguzi.
Kwamba ni mjadala wa Kitabaka na kuwa Zitto na January sio tabaka stahili la
vijana walio wengi. Sitamsemea January, nitajibu baadhi ya hoja za mwandishi wa
makala mojawapo kama Zitto. January akitaka atamjibu naye kivyake.
Mwandishi anasema yeye
hapingi hoja ya umri, bali anapinga aina ya watu wanaoshadidia hoja hiyo.
Anaipenda hoja ila hapendi watoa hoja. Hoja nzuri lakini Zitto na January
wabaya. Amelisema hilo mwanzo kabisa wa makala yake. Kwa hiyo kwake yeye hoja
ingeletwa na vijana wengine asingekuwa na shida wala isingekuwa hoja hatari.
Kwa kuwa hoja imeletwa na Zitto na January (ingawa sisi sio waanzilishi wa hoja
hii) ni hoja ya kibaguzi. Nawashangaa sana wasomi wa siku hizi. Wasomi
wanaojadili watu badala ya masuala.
Mahojiano na Anna Mwalagho
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Kazi yetu ni kutunza kumbukumbu za wale ambao wanathamini mawazo fikra, mbinu
zao kwa manufaa yawengine au vizazi vipya.
Msikilize kwa makini Muigizaji, Mchezaji, Mshairi, msimulizi wa hadithi na mwimbaji Anna Mwalagho akieleza mengi kuhusu maisha yake. Ameeleza alivyoanza mpaka alipofikia, waliomvutia, mafanikio katika kazi na mengine mengi.
Msikilize kwenye mahojiano haya aliyofanya nasi ndani ya studio za Asparagus zilizopo Takoma Park, jimbo la Maryland nchini Marekani
Msikilize kwa makini Muigizaji, Mchezaji, Mshairi, msimulizi wa hadithi na mwimbaji Anna Mwalagho akieleza mengi kuhusu maisha yake. Ameeleza alivyoanza mpaka alipofikia, waliomvutia, mafanikio katika kazi na mengine mengi.
Msikilize kwenye mahojiano haya aliyofanya nasi ndani ya studio za Asparagus zilizopo Takoma Park, jimbo la Maryland nchini Marekani
Balozi wa Ireland atembelea Kiwanda cha bia cha Serengeti (SBL)
Sunday, March 25, 2012 Maoni:
0
Balozi wa Ireland
nchini Tanzania Mhe. Loscan Fullan (katuikati) akimsikiliza Brewery Manager wa
SBL Colman Hanna juu ya hatua mbalimbali za uzalishaji bia SBL. Kulia ni Meneja
wa Fedha na Biashara wa SBL, John Collins.
Balozi wa Ireland
nchini Tanzania Mhe. Loscan Fullan (kushoto) akitoka baada ya kumaliza ziara
hiyo kiwandani hapo. Pamoja nae ni Brewery Manager wa Kampuni ya Bia ya
Serengeti (SBL) Colman Hanna na Meneja wa Fedha na Biashara wa SBL, John
Collins anaeonekana kwa nyuma.
Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mhe. Loscan
Fullan (wapili kulia) Meneja wa Fedha na Biashara wa SBL, John Collins, Brewery
Manager wa SBL Colman Hanna, Meneja Mawasiliano wa SBL, Imani Lwinga na
Meneja wa Ubora wa SBL, Alloyce Nduka wakionja bia za SBL wakati wa ziara hiyo
ya Balozi.
Balozi wa Ireland
nchini Tanzania Mhe. Loscan Fullan (kushoto) akitembezwa katika kiwanda na
Meneja wa Fedha na Biashara wa SBL, John Collins (kulia) na Brewery Manager wa
SBL Colman Hanna. MBIO ZA KUMPATA MISS UTALII KINONDONI 2012 ZAANZA
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Miss Tourism Tanzania Organization – Kinondoni, wenye dhima ya
kikomo ya kuandaa na kuendesha mashindano ya Miss Utalii Kinondoni,wametangaza
nafasi kwa mabinti wenye sifa za kushiriki Miss Utalii Kinondoni 2012
kujitokeza kujaza fomu za kuomba kushiriki mashindano hayo,yaliyopangwa
kufanyika mwishoni mwa Aprili 2012 wilayani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini, mkurugenzi wa Miss
Tourism Tanzania Organisation wilaya ya Kinondoni,Ndugu Pius Yalula, amesema
kuwa fomu hizo zitaanza kutolewa siku ya Jumatatu Tarehe 26-3-2012 katika
maeneo mbalimbali Jijini Dar es Salaam. Baadhi ya maeneo hayo ni pamoja na
Zizzu Fashion ( Victoria) ,BM Saloon ( Kinondoni), Sea Boys Internet Café (
Magomeni), Aucland Tours & Safaries ( Maeneo ya Posta), Ofisi za Mlonge By
Makao ( Pamba House Posta), Katika Ofisi za Miss Tourism Tanzania Organization
( Ilala Bungoni), Dar es Salaam City Collage ( Kimara), Kumekucha Action Mart
(Sinza)COCO Beach Oyster bay na TINTONA TANKSTATION ( Kinondoni Manyanya).
Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu hizo ni tarehe 12-4-2012, kabla ya kuanza
kwa kambi ya mazoezi kati kati ya mwezi huo April 2012.
Mkurugenzi huyo wa wilaya wa mashindano hayo,alibainisha kuwa sifa
za washiriki kwa mujibu wa kanuni na Taratibu za mashindano ya Miss Utalii
Tanzania ni pamoja na , washiriki kuwa na Elimu isiyo pungua kidato cha sita au
yenye kulingana nayo, umri usio pungua miaka 18-27, Urefu wa angalau sentimita
168 au zaidi, wenye rangi na maumbile asili, Wenye afya njema kimwili na
kiakili, wasio olewa wala kuwahi kuzaa, raia wa Tanzania kwa mujibu wa sheria.
Wenye tabia njema,mwenendo mwema , mfano wa kuigwa na tegemeo katika jamii kimaadili
na hulka.
Washindi wa shindano hilo watawakilisha na kupepelusha Bendera ya
Wilaya ya Kinondoni katika fainali za mkoa wa Dar Es Salaam ,
zitalazo wakutanisha washindi hao na washindi wenzao wa wilaya za Ilala na
Temeke zitakazo fanyika mwishoni mwa mwezi Mei 2012, wakichuana kuwania taji la
Miss Utalii Dar Es Salaam 2012. Jumla ya warembo 24 watashiriki fainali za Mkoa
wa Dar es Salaam, ikiwa ni nane kutoka kila wilaya.
Kwa niaba ya kamati ya maandalizi wilaya ya Kinondoni 2012, natoa
wito kwa mabinti wenye sifa na uzalendo wa dhati kwa wilaya,mkoa na taifa kwa
ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki, ikiwa ni fulsa ya pekee kwao kuunga
mkono juhudi za serikali na Taifa katika kutangaza na kuhamasisha
Utalii,Utamaduni,Matumizi ya Bidhaa za na Huduma za Tanzania, Mianya ya
Uwekezaji na pia kuhamasisha vita dhidi ya Uharibifu wa Mazingira,Uwindaji
Haramu,Uvuvi Haramu,Ujinga,Umasikini, Maradhi, Mila kongwe na Potofu.
Aidha tunaomba watu binafsi, makampuni na mamlaka za serikali za
Wilyaya ya Kinondoni kujitokeza kudhamini shindano hili,likiwa ni shendano
pekee nchini lisilo husisha mavazi ya kuogelea ,wala mavazi yasiyo ya asili ya
Tanzania ambalo litatoa fulsa ya pekee kwa wafanya bishara,makampuni na Wilaya
kujitangaza kiuchumi,kitalii,kiuwekezaji na kijamii kitaifa na kimataifa.Miss
Utalii Tanzania ni Alama ya Urithi wa Taifa, hazina na benki kubwa ya Utamaduni
wa Tanzania kwa faida ya sasa na baadae.
Wilaya ya Kinondoni , ndiyo inayo shikilia taji la Miss Utalii Dar
es Salaa 2011, na taji la Miss Utalii Tanzania 2011 – Mshindi wa Tano, ambapo
Mrembo Sofia Dio ndiye anaye shikilia mataji hayo na ndiye atakaye kabidhi taji
kwa mrembo mpya wa Miss ?Binti Utalii Kinondoni 2012.
Asante,
Pius Yalula
Mkurugenzi Miss Utalii Kinondoni
Nakala:
Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano Miss Tourism Tanzania
Organisation
Uandishi wa Kitabu cha Marehemu Regia Mtema (Biography)
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Kamati Teule iliyochaguliwa kuanzisha Taasisi
ya Regia Mtema Foundation imedhamiria kufuatilia kuandikwa kwa kitabu cha
Marehemu Regia Mtema kufuatia azimio lililoafikiwa katika kikao cha kwanza cha
Marafiki wa Regia pale British Council na baadaye kuwekewa uzito katika kikao
cha Kamati Teule.
Kamati
Teule sasa inapenda kutoa fursa ya kualika mtu au kampuni yeyote ambayo inaweza
kuifanya kazi hiyo ya uandishi kwa uharaka, ustadi na ubora wa hali ya juu.
Itahitajika kujua mchanganuo wa gharama zote za zoezi zima.
Kazi
hii inatarajiwa itahusisha kuweka kumbukumbu ya historia ya Regia, Kazi
mbalimbali alizofanya, picha nk. nk.
Kama wewe ni mojawapo wa waandishi wa
Biography au unamfahamu yeyote, tafadhali naomba tuwasiliane moja kwa moja
kupitia barua pepe sam@danimex.com.
Application Open for a Film Master Class Workshop
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Dear alumni and
filmmaking friends!
Please forward
this mail to anyone you may know who may benefit from our Masterclass
Filmmaking Workshops.
We want the
widest range of applications possible. Pls support us support your community.
Pay it forward & send this to everyone you know!!!!!!
Dear all
A reminder we are open for applications for
our annual Master
class Film Training Workshops. www.onefinedayfilms.com
This is our fourth year! There
are two aspects.
1. The 2 week Master Class Classroom Filmmakers Workshops.
These are June 18th to June 29th
2012.
They have previously been held in Kenya, for the 60 participants invited to attend from all
over Africa. This year we may be hosting the
workshops in another location (Zanzibar, Kampala,
Arusha, Kigali are being considered).
We cover all travel and accommodation costs for successful candidates. There is no charge for the course.
There are EIGHT departments
1.
Cinematography
2. Directing
3. Editing
4. Film
composing (NEW!!!!)
5. Production
6. Production
design / art department
7.
Scriptwriting
8. Sound
These classes are conducted by world
class filmmakers from Europe and the USA (last year we had a
delegation from the Oscars who came to teach)
2. The Feature film. This
will be shot October / November 2012. It is a 4 week shoot.
Priority for all crew selected is given to
those attending the two week classroom workshop. We are not yet confirmed which
country we will shoot in, but it will likely be Kenya.
This is a Master class training so
you should have an armful of experience to apply, and you must attend all
days. And
you cannot possibly be too experienced!
The application consists of THREE PARTS:
1. A
completed Application Form to be emailed to application@onefinedayfilms. org
2. A 1 minute
application video about yourself uploaded to YouTube (the URL of
uploaded content to be stated in the Application Form).
3. A1 minute
application video on your previous work, work sample, show reel, etc uploaded
to YouTube (the URL of uploaded content to be stated in the Application
Form).
Application forms are available on. www.onefinedayfilms.com
Closing date 25th March. Only
complete applications will be considered.
Email us if you have any questions – but
please do not send me your application forms and materials!
Lastly please pass this on to your
filmmaker friends all over Africa.
Remember - we will cover all travel costs
for participants and want this to be a truly Pan African programme.
Thanks!
wizar ya afya yaimarisha hatua mbalimbali za kudhibiti maambukizi shirikishi ya kifua kikuu na ukimwi
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Na. Catherine
Sungura-Masasi
24/03/2012
TB-Kitaifa.
Wizara ya Afya na Ustawi
wa Jamii imeimarisha hatua mbalimbali za kudhibiti maambukizi shirikishi ya
kifua kikuu na ukimwi ikiwa ni pamoja na kuchunguza kila mgonjwa wa kifua kikuu
kama ana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi(VVU) katika kila kituo cha afya na
hospitali zote nchini.
Hayo yamesemwa leo na
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hadji Mponda kwenye hotuba yake kwenye
Kilele cha maadhimisho ya siku ya kifua kikuu duniani yaliyofanyika wilayani
hapa. Dkt. Mponda alisema katika kutekeleza hilo wizara yake inafanya
uchunguzi, kutoa dawa ya kuzuia kifua kikuu kwa watu wanaoishi na VVU pamoja na
dawa za mseto za kutibu kifua kikuu hivyo kupunguza muda wa matibabu kutoka
miezi nane hadi sita .
Alisema asilimia 88 ya
wagonjwa wote wa kifua kikuu wanapona baada ya kupata matibabu sahii kwa
kutumia dawa mseto,kiwango hicho ni zaidi ya lengo la Shirika la Afya Duniani
ambalo linataka kila mwanachama kuponyesha angalau asilimia 85 ya wagonjwa wa
kifua kikuu, “hivyo sehemu kubwa wagonjwa wa kifua kikuu wanao uhakika wa
kupona baada ya kuanza matibabu hata kama pia wana maambukizi ya VVU.
Hata hivyo alisema
Wizara imeanza kununua na kusambaza aina mpya ya darubini za Light Emitting
Diode(LED) zenye uwezo mkubwa zaidi wa kugundua vimelea vya kifua kikuu katika
makohozi, hadi kufikia mwisho wa mwaka jana asilimia 80 ya hospitali zote za
wilaya zilipata darubini hizo mpya na ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, hospitali
zote zikiwemo za mashirika ya kidini zitapatiwa lengo ni kuzipa hospitali zote
nchini uwezo mkubwa wa kuchunguza vimelea vya kifua kikuu.
“ Ninaomba watoa huduma
kuhakikisha kwamba kila mgonjwa wa kifua kikuu anachunguzwa maambukizi ya VVU
baada ya kupata ushauri nasaha na hivyo hivyo wenye maambukizi ya VVU
wachunguzwe pia ugonjwa wa kifua kikuu na wale wote watakaobainika wana
maambukizi shirikishi wapewe matibabu sahii ikiwemo dawa za kupunguza makali ya
virusi mapema iwezekanavyo kulingana na mwongozo wa Wizara”alisisitiza.
Aidha Dkt. Mponda
alisema kwa kauli mbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya kifua kikuu “
Nitatokomeza kifua kikuu kipindi chote cha uhai wangu” ina lenga watoto ambao
ni taifa la kesho wategemee kuishi kwenye ulimwengu ambao hakuna mtu yeyote
anaugua kifua kikuu hivyo swala la kutokomeza ugonjwa huu si la Wizara ya Afya
na Ustawi wa Jamii peke yake bali ni la kushirikisha sekta zote hapa nchini.
Awali Kaimu Mganga Mkuu
wa Mkoa wa Mtwara Dkt. Ernest Kasoyaga alisema ugonjwa wa kifua kikuu bado ni
tatizo kubwa mkoani hapo ambapo takwimu zinaonyesha idadi kubwa ya wagonjwa
waliogunduliwa na kupatiwa matibabu mwaka 2009 kulikuwa na wagonjwa (1,902) ,
mwaka 2010 (1,898), mwaka 2011 (1,907) , na katika wiki hii ya maadhimisho kwa
siku sita waliendesha zoezi la kuhamasisha na kupima makohozi kwa wananchi wa
wilaya ya masasi katika vituo saba, ambapo watu wapatao 602 waliojitokeza
katika zoezi hilo wakiwemo wanaume 287 na wanawake 315 kati ya watu hao watu 25
waligundulika kuwa na vimelea vya kifua kikuu idadi hiyo ni sawa na asilimia
3.6.
Alisema ongezeko hilo la
wagonjwa linatokana na maambukizo ya VVU ambapo toka oktoba mwaka 2010 hadi
Septemba 2011 kati ya wagonjwa wa kifua kikuu 1,647 waliopimwa VVU, wagonjwa
440 sawa na asilimia 27 waligundulika na Virusi vya Ukimwi.
Rais Kikwete awaapisha Makatikbu Tawala wa Mikoa ikulu jijini Dar Es Salaam
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Katibu Tawala mpya wa mkoa wa Mbeya Bibi.Mariam
Mtunguja akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar
es salaam leo.Katika hafla hiyo Rais aliwaapisha pia makatibu Tawala wa mikoa
mingine kama ifuatavyo,Dkt. Faisal Issa(Kilimanjaro),Bwana Eliya
Ntandu(Morogoro), Bwana Severine Kahitwa(Geita),Bwana Emmanuel
Kalobelo(Katavi), Bwana Hassan Bendeyeko(Ruvuma) na Dkt. Anselem Tarimo
(Shinyanga)(Picha na Freddy Maro).
serikali ya china yaipa mkopo nafuu na msaada Tanzania zaidi ya bilioni 80
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Naibu Waziri wa Biashara wa
China Li Jinzao (kulia ) akisaini kitabu cha wageni cha Wizara ya Fedha leo
jijini Dar es salaam wakati alipokwendakusaini mkopo na misaada kutoka
Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa ajili ya kuisaidia Tanzania katika
miradi mbalimbali inayozidi shilingi bilioni 80. Sherehe hizo zilisainiwa na
Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo(hayupo pichani)kwa niaba ya Tanzania na Naibu
Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao
Waziri wa Fedha
Mustafa Mkulo(kushoto) na Naibu Waziri wa Biashara wa China Li Jinzao (kulia)
wakisaini makubaliano leo jijini Dar es salaam ya Serikali ya China kuipa mkopo
nafuu na msaada kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo nchini. Msaada na
mikopo hiyo ni zaidi bilioni 80 fedha za Kitanzania ambayo inazidi kuimarisha
urafiki na undugu kati ya Tanzania na China.
Naibu Waziri wa Biashara wa
China Li Jinzao (aliyesimama ) akitoa hotuba jana jijini Dar es salaam wakati
wa sherehe fupi ya kusaini mkopo na misaada kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu
wa China kwa ajili ya kuisaidia Tanzania. Sherehe hizo zilisainiwa na Waziri wa
Fedha Mustafa Mkulo (hayupo pichani)kwa niaba ya Tanzania na Naibu Waziri wa
Biashara wa China Li Jinzao. Kulia ni Balozi wa China nchini Lu Youqing.
Waziri wa Fedha Mustafa
Mkulo(aliyesimama ) akitoa hotuba jana jijini Dar es salaam wakati wa sherehe
fupi ya kusaini mkopo na misaada kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Sherehe hizo zilisainiwa na Waziri Mkulo kwa niaba ya Tanzania na Naibu Waziri
wa Biashara wa China Li Jinzao (hayupo pichani) . Msaada na Mkopo huo unazidi
bilioni 80 Fedha za Kitanzania. Kushoto ni Waziri wa Uchukuzi Omar Nundu na
kulia ni Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja.
Waziri wa Fedha Mustafa
Mkulo(kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Biashara wa China
Li Jinzao (kulia) leo jijini Dar es salaam wakati kiongozi huyo alipokwenda
Wizara ya Fedha kwa ajili ya kusaini mkataba wa mkopo nafuu na msaada wa zaidi
ya bilioni 80 za Kitanzania kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za
maendeleo nchini.
KAMPUNI YA ALLIANCE ONE TANZANIA YAWAELIMISHA WAHARIRI JUU YA ZAO LA TUMBAKU
Saturday, March 24, 2012 Maoni:
0
Mkurugenzi wa Alliance One Tanzania Ltd Bw. Mark Mason akizugumza
katika mkutano na wahariri wa vyombo mbali mbali vya habari jijini Dar es
Salaam. Mkutano huo uliandaliwa kwa ajili ya kuwapa taarifa juu ya maendeleo ya
tumbaku na mambo mbali mbali wanayoyafanya katika kuisaidia jamii. Kampuni hiyo
inafanya shughuli za Tumbaku huko Kinglowila, Morogoro.
Meneja Uhusiano wa Alliance One Tanzania Ltd, Bw. Hamis Liana
akiwaeleza wahariri juu ya miradi mbali mbali ya kijamii inayotolewa na kampuni
yao kupitia zao la tumbaku ambalo wanashughulikia huko mkoani Morogoro. Mkutano
huo ulifanyika leo jijini Dar es Salaam.
Wahariri kutoka The African Bw. Shermax Ngahemera, Uhuru Bw. Damas
na Bethuel Kinyori wa Corporate Digest na Meneja Uhusiano wa Silverbullet PR
Nadine Kapya wakiwa katika mkutano na Alliance One Tanzania Ltd jijini Dar es
Salaam.
Michuzi Jr

Kumbu Kumbu
BLOG MBALI MBALI
VYOMBO VYA HABARI
TANZANIA HOUSE OF TALENTS

Computer Problems?

Clouds FM
BLOG IMETENGENEZWA NA:
·
Blogger
news
·
Blogroll
·
About
·
Labels
·
.
(1)
Copyright © 2011 MICHUZI
JR. All rights reserved.
Jiachie
Blog V2 | Modified by MKCT








































0 Comments