Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Aagiza Kampuni ya Ujenzi ya Electric International Company Limited Kukamilisha Ujenzi wa Skuli Mpya ya Sekondari ya Wilaya ya Kusini iliyopo Paje Mtule Vinginevyo itafukuzwa na italazimika Kulipa Gharama Zote Zitakazojiri Kuitia Hasara Serikali Ya Mapinduzi Zanzibar
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akikagua Jengo la
Ofisi ya Elimu Wilaya ya Kusini liliopo Makunduchi likikaribia hatua ya
uwezekaji ambapo aliahidi kuchangia Matofali 3000 na Mifuko ya Saruji
30 kukamilishia ujenzi huo.
Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Abdulla Mzee
Abdulla akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Iddi kuhusu ucheleweshaji wa ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya
Wilaya ya Kusini iliyopo Paje Mtule. Balozi Seif aliagiza kufutwa mara
moja kwa mkataba wa ujenzi na kampuni ya Electric International endapo
hatokamilisha ifikapo mwishoni mwa mwezi wa julai mwaka huu
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliangalia Darasa la
Kompyuta la Charity School iliyopo Bwejuu baada ya kuweka jiwe la
Msingi la Skuli hiyo.Kulia ya Balozi ni Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Mh.
Mohd Ibrahim, Naibu Waziri wa Elimu Mh. Zahara Hamad pamoja na Baadhi
ya Waalimu wa Skuli hiyo ya Maandalizi na Msingi.
0 Comments