
Picha za video zinazorusha mkutano huo zimewaonyesha marais hao wakiwa katika jukwaa moja wakipiga picha baada ya kumaliza majadiliano ya sehemu ya kwanza.
Katika upigaji picha, Rais Kikwete ameonekana akiwa ameketi mwanzo akiwafuatiwa na rais wa Nigeria, Obasanjo na kisha kufuatiwa na Mahamud wa Somalia. Rais Mkapa ameketi nafasi ya nne akifuatiwa na kiongozi mwingine ambaye hakuweza kutambulika mara moja na mwishoni aliketi Rais Thabo Mbeki ambaye taasisi yake ndiyo mwenyeji wa mkutano huo.
Mara baada ya kumalizika kwa shughuli ya upigaji picha, Rais Kikwete alionekana akijadiliana jambo kwa karibu na Rais Obasanjo na kisha viongozi hao waliteremka kutoka jukwaani.
Wakati akielekea kwenye eneo lake Kikwete aliwasalimia wageni kadhaa ndani ya mkutano huo na baadaye alielekea sehemu aliyokuwa amesimama aliyekuwa katibu mkuu kiongozi, Ombeni Sefue na kuonekana akimsisitizia jambo na kisha akaondoka.
Viongozi hao wamekuwa wakijadiliana kuhusu masuala ya demokrasia, utawala bora na jinsi ya kuzisaidia nchi za Afrika kusonga mbele kimaendeleo.
0 Comments