Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,William Lukuvi(kulia)akiwasili kwenye makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Arusha,iliyopo wilayani Arumeru katika ziara yake ya siku tatu na ujumbe wake.
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,William Lukuvi akizungumza na wakazi wa wilaya ya Arumeru kwenye viwanja vya halmashauri ya Arusha eneo la Sekei,alipata fursa ya kusikiliza kero za mashamba ambayo aliahidi kuifanyia kazi,kulia ni Mpima Ramani mkoa wa Arusha,Hamduni Mansoor na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Agatha Msuya.
Mzee Alfred Lekshon mkazi wa wilaya ya Arumeru akimweleza Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,William Lukuvi jinsi alivyonyang’anywa shamba lake lenye ukubwa hekari 25.
Mkazi wa Olosiva ,wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha,ambaye ni mjane Mwanahamisi Almasi akisimulia kero anazozipata kutoka kwa mtu anayetaka kumnyang’anya nyumba na kiwanja chake na kuwa amekua akisumbuliwa na kutishiwa .
Mwekezaji ambaye kutoka nchini Denmark,Finn Petersen ambaye kutokana na migogoro ya ardhi ameshindwa kuendelea na uwekezaji wake eneo la Oljoro baada ya eneo lake kuvamiwa na wananchi.
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha,Juma Idd(katikati)akifafanua jambo wakati akieleza mpango wa kutekeleza mradi wa kuliweka Jiji la Arusha katika hadhi ya kimaita utakaotekelezwa hivi karibuni,kulia ni Mpima Ramani wa mkoa wa Arusha,Hamduni Mansoor.
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,William Lukuvi(kushoto)akipata ufafanuzi wa mojawapo wa majalada kwenye ofisi ya Masjala ya Ardhi kutoka Afisa Ardhi Mteule wa halmashauri ya wilaya ya Arusha,Rehema Mdee .
Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Arusha,Agatha Msuya akizungumza kwenye mkutano wa wananchi kueleza kero za mashamba na viwanja kwa Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Meya wa Jiji la Arusha,Gaudence Lyimo akizungumza na wananchi kwenye viwanja vya Makumbusho ya Taifa wakati wa mkutano wa Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,William Lukuvi kusikiliza kero za wananchi.Picha zote na Muungano Saguya.









0 Comments